
Na Mwandishi Wetu, Bunda
-------------------------------------
-------------------------------------
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mara kwa kushirikiana na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini, limekamata magunia 205 (pichani juu) yakiwa na majani makavu yanayodhaniwa kuwa zao haramu la bangi.
Aidha, jeshi hilo linawashikilia watu wawili waliokutwa wakisafirisha magunia hayo kwenye gari la mafuta kutoka mkoani Mara kwenda jijini Dar es Salaam.
Ukamataji huo ulifanyika wilayani Bunda jana, ambapo Mkuu wa Wilaya hiyo, Dkt Vicent Naano alikemea uhalifu huo akisema mamlaka zimejipanga kuwadhibiti wakulima, wasafirishaji na wafanyabiashara ya dawa za kulevya mkoani Mara.
UNAWEZA PIA KUSOMA:
- 1.Mfanyabiashara tajiri zaidi Afrika awashangaza wengi umiliki wa nyumba.
- 2.Simiyu: Wananchi wazuia mabasi ya abiria Nyamikoma, baadhi yadaiwa kupondwa mawe.
- 3.Tarime Sekondari yang'ara tena Matokeo ya Mtihani Kidato cha Sita.
- 4.Hispania yashinda Euro tena kwa mara ya nne.
- 5.Rais Samia avutiwa Hifadhi ya Katavi, aahidi kufanya ‘royal tour’ ya kuitangaza.
No comments:
Post a Comment