
Rais William Ruto
--------------------------
Rais wa Jamhuri ya Kenya, William Ruto amewateua baadhi ya viongozi wa upinzani kuingia katika Baraza lake jipya la Mawaziri.
Ruto pia amewarejesha mawaziri wa zamani wanne waliokuwa katika Baraza lake la awali, akiwemo aliyekuwa Mkuu wa Sheria, Justin Muturi.
Mawaziri walioteuliwa kutoka vyama vya upinzani kikiwemo ODM na wizara zao zikiwa kwenye mabano, ni pamoja na Hassan Joho (Madini), John Mbadi (Fedha), Stella Langat (Jinsia) na Wycliffe Oparanya (Vyama vya Ushirika).
Mbali na hao wa upinzani, wengine walioteuliwa kuwa mawaziri katika Baraza jipya la Rais Ruto, ni Salim Mvurya (Uwekezaji), Rebecca Miano (Utalii), (Opiyo Wandayi (Nishati), Kipchumba Murkomem (Vijana na Michezo), Alfred Mutua (Kazi) na Justin Muturi (Utumishi wa Umma).
UNAWEZA PIA KUSOMA:
- >>Mwenyekiti CCM Mara:Tumejipanga vizuri kuupokea Mwenge wa Uhuru kesho
- >>Mwenge wa Uhuru kuwasili Mara kesho, kukagua miradi ya bilioni 25/-
- >>TIC watembelea kahawa ya Tarime inayotamba soko la dunia
- >>Nyambari akutana na Spika wa Bunge la Tanzania jijini New Delhi
- >>Mwenyekiti UWT CCM Mara ahamasisha wanawake wilayani Tarime kugombea uongozi, wavuna wanachama wapya
- >>Balozi Mbarouk amwandikia Spika barua ya kujiuzulu ubunge
- >>Maswi, Ridhiwan wang’ara teuzi za Rais Samia, Nape na Makamba wavuliwa uwaziri, Mashinji na Afraha wahamishwa Serengeti
No comments:
Post a Comment