Korea Kusini imemwita balozi wa Urusi, ikitaka "kuondoka mara moja" kwa wanajeshi wa Korea Kaskazini ambayo inasema wanapewa mafunzo ya kupigana nchini Ukraine.
Takriban wanajeshi 1,500 wa Korea Kaskazini, wakiwemo wale wa kikosi maalum tayari wamewasili nchini Urusi, kwa mujibu wa shirika la kijasusi la Seoul.
Takriban wanajeshi 1,500 wa Korea Kaskazini, wakiwemo wale wa kikosi maalum tayari wamewasili nchini Urusi, kwa mujibu wa shirika la kijasusi la Seoul.
Katika mkutano na balozi Georgiy Zinoviev, makamu wa waziri wa mambo ya nje wa Korea Kusini Kim Hong-kyun alishutumu hatua hiyo na kuonya kwamba Seoul "itajibu kwa hatua zote zinazowezekana".
Bw Zinoviev alisema atawasilisha jambo hilo, lakini akasisitiza kuwa ushirikiano kati ya Moscow na Pyongyang "uko ndani ya mfumo wa sheria za kimataifa".
Haijulikani alikuwa akimaanisha ushirikiano gani. Balozi huyo hakuthibitisha madai kuwa Korea Kaskazini imetuma wanajeshi kupigana na jeshi la Urusi.
Pyongyang pia haijazungumzia madai hayo.Korea Kusini kwa muda mrefu imekuwa ikiishutumu Kaskazini kwa kusambaza silaha kwa Urusi kwa ajili ya matumizi katika vita dhidi ya Ukraine, lakini inasema hali ya sasa imevuka uhamishaji wa vifaa vya kijeshi.
Baadhi ya ripoti za vyombo vya habari vya Korea Kusini vimesema kuwa wanajeshi 12,000 wa Korea Kaskazini wanatarajiwa kutumwa. "Hii sio tu inatishia sana Korea Kusini lakini jumuiya ya kimataifa," Kim alisema Jumatatu.
Moscow na Pyongyang zimeongeza ushirikiano baada ya viongozi wao Vladimir Putin na Kim Jong Un kutia saini mkataba wa usalama mwezi Juni, wakiahidi kuwa nchi zao zitasaidiana iwapo kutatokea "uchokozi" dhidi ya nchi yoyote ile.
UNAWEZA PIA KUSOMA:
>>Watu wanane waripotiwa kufariki dunia katika ajali ya mabasi Mwanza
>>MAKALA:Nyambari Nyangwine awapa vijana misingi ya kujenga taifa akihutubia mahafali ya kidato cha nne Mbezi High School
>>Serengeti, Mlima Kilimanjaro zaendelea kuiheshimisha Tanzania kimataifa
>>MAKALA MAALUMU:Tunamuenzi Mwalimu Nyerere kwa kuwafikishia wananchi huduma ya maji, hakuna atakayeachwa
No comments:
Post a Comment