
Stephen Masato Wasira
Na Mwandishi Wetu/ Mara Online News
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira, leo Jumatatu anaanza ziara ya kikazi mkoani Mara.
Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Idara ya Uenezi ya CCM Mara, Wasira atatembelea wilaya zote sita za mkoa huo, akianzia wilaya ya Bunda.
Hiyo itakuwa ziara yake ya kwanza mkoani Mara tangu achaguliwe na Mkutano Mkuu wa CCM Taifa hapo Januari 18, 2025 kushika madaraka hayo.
Wasira ni mmoja wa wanasiasa mashuhuri tangu enzi za kudai uhuru wa Tanganyika miaka ya 1950.
Amewahi kushika nyadhifa mbalimbali serikalini tangu awamu ya kwanza ya uongozi wa Mwalimu Julius Nyerere.
Baada ya kuchaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Wasira alisema jukumu lake kubwa litakuwa kuimarisha chama hicho tawala ili kiendelee kushika dola.
UNAWEZA PIA KUSOMA:
>>Mara: HAIPPA PLC yapokea wanahisa wapya zaidi ya 300, yanadi huduma zake
>>Ajali ya ndege Marekani yaua watu 67 wakiwemo wanajeshi
>>Sekondari ya Tarime Mchanganyiko yang’ara matokeo kidato cha nne 2024
>>Serengeti na Ngorongoro: Serikali ya Ujerumani, TANAPA, FZS wazindua miradi ya kijamii iliyogharimu mamilioni ya fedha
No comments:
Post a Comment